<?xml version="1.0" ?>
<rss version="2.0">
<channel>
<description> </description>
<link>http://www.ipsinternational.org/africa/sw/</link>
<title>  IPS Swahili  </title>
<managingEditor>mgutierrez@ips.org (Miren Gutierrez)</managingEditor>
<webMaster> newsletters@ipsnews.net (Walter Garcia)</webMaster>
<language>SW-sw</language>
<image>
<title>  IPS Swahili  </title>
<url>http://www.ipsinternational.org/africa/sw/../../logo_ips.gif</url>
<link>http://www.ipsinternational.org/africa/sw/</link>
<width>100</width>
<height>42</height>
</image>
<item>
<title>
Mauritania: Hatua Ndogo za Kutokomeza Tohara kwa Wanawake
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4067
</link>
<description>
NOUAKCHOTT&#044; Mei 8 &#040;IPS&#041; &#045; Mkakati mkali wa kukomesha tohara kwa wanawake 
nchini Mauritania unaleta mafanikio ya polepole, pamoja na kwamba 
wanaharakati wanatambua bado kuna mambo mengi ya kufanyika katika 
taifa ambalo theluthi mbili ya wasichana wamefanyiwa tohara. 

</description>
</item>
<item>
<title>
GHANA: Akina Baba Wapambana Kuwaokoa Watoto Wao wa Kike Kutokana na Tohara
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4066
</link>
<description>
ACCRA&#044; Mei 8 &#040;IPS&#041; &#045; Wakati Jack Sabadgou alipoondoka nchini Ghana 
kwenda Uswis miaka 10 iliyopita, aliacha mtoto mchanga wa kike 
nyuma ili aweze kulelewa na mama yake. Sasa anahitaji kuishi na 
mtoto wake, na mwanaume huyo anaona muda haumtoshi kumwokoa mtoto 
wake kutumbukia kwenye mila zilizopigwa marufuku za tohara kwa 
wanawake na watoto wa kike. 
</description>
</item>
<item>
<title>
TANZANIA: Ufugaji Viumbe Bahari, Muhimu Kuongeza Kipato, Kutunza Mazingira
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4065
</link>
<description>
BAGAMOYO&#044; Mei 7 &#040;IPS&#041; &#045; Kwa miaka mingi wakazi wa pwani wamekuwa 
wakitegemea zaidi kujipatia kipato na chakula kutokana na 
kuendesha shughuli za uvuvi aidha katika mabwawa au kwenye Bahari 
ya Hindi. &quot;Lakini kutokana na kuongezeka kwa watu samaki 
wamepungua kwa kiasi kikubwa katika bahari na katika mabwawa ya 
asili na mahitaji yamezidi kuongezeka,&quot; alisema Mkurugenzi wa 
Mradi wa Pwani wa Mpango wa Kusimamia Mazingira na Rasilimali za 
Pwani (TCMP &#8211; Pwani), Baraka Kalangahe. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Kuokoa Maisha ya Akina Mama katika Sudan Kusini
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4064
</link>
<description>
JUBA&#044; Mei 7 &#040;IPS&#041; &#045; Martha Borete Angela ni mwanafunzi wa mwaka wa 
kwanza katika programu ya wakunga wa jadi katika Taasisi ya 
Mafunzo ya Afya ya Sudan Kusini. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Dharula Iliyosahauliwa katika Jimbo la Blue Nile Nchini Sudan
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4063
</link>
<description>
JAMAM, Sudan Kusini&#044; Mei 7 &#040;IPS&#041; &#045; Hamid Yussef Bashir alisema alitembea kwa siku 17 
na mke wake na watoto watano ili kufika katika kambi ya wakimbizi 
katika Sudan Kusini. Walipofika Jamam, waliungana na watu wengine 
wapatao 37,000 ambao walikimbia vita na hivyo kuwafanya kuvuka 
mpakani katika jimbo la Blue Nile nchini Sudan. 
Mazingira ya 
kambi ya wakimbizi hayafai, alisema. Kuna uhaba wa maji safi na 
familia yake inabidi kuhamisha kibanda chao kabla mvua haijaanza 
kunyesha na mafuriko kulikumba eneo waliloweka kambi. Lakini 
walikuwa na bahati kuweza kusafiri salama hadi hapa. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Njaa Nchini Chad: Wanawake  Wavunja Vichuguu Kutafuta Nafaka Zilizohifadhiwa na Mchwa
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4062
</link>
<description>
N&#8217;DJAMENA&#044; Mei 7 &#040;IPS&#041; &#045; &quot;Ni Mungu tu anayejua nini kinatokea kwangu 
mimi na watoto &#8211; kwa miezi miwili hatukuwa na kitu cha kula. 
Tunaishi kama ombaomba,&quot; Henriette Sanglar, mama wa watoto 
wanne katika majengo ya makazi ya Moursal kwenye mji mkuu wa 
Chad, N&#8217;Djamena, aliiambia IPS. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Watoto wa Ivory Coast Waishi kwa Hofu
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4061
</link>
<description>
ABIDJAN&#044; Aprili 23 &#040;IPS&#041; &#045; Kundi la watoto wanaocheza katika eneo la wazi 
kwenye mji maarufu kibiashara wa Ivory Coast wa Abidjan 
wanaonekana kutokuwa na uangalizi. Lakini gari linapotoa ngurumo 
mkali na kutoa moshi, wanatetemeka. Wakati askari wanapotembea 
kupita eneo hilo, wanatetemeka. Na wanaonekana kuwa na hofu 
wakati mtu mzima anapowasogelea. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Jukwaa la Maji Duniani Lasema Mabwawa Makubwa &#8216;Siyo Endelevu&#8217;
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4059
</link>
<description>
MARSEILLE, Ufaransa &#044; Aprili 23 &#040;IPS&#041; &#045; Mashirika kadhaa yasiyokuwa ya kiserikali yalitumia 
Jukwaa la Maji Duniani (WWF) lililofanyika mjini Marseille wiki 
iliyopita kama fursa ya kukumbusha jumuiya ya kimataifa kuhusu 
madhara makubwa ya mabwawa makubwa duniani kote. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Maji Yanapokauka Katika Mabomba ya Mauritius
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4058
</link>
<description>
PORT-LOUIS&#044; Apirili 23 &#040;IPS&#041; &#045; Rani Murthy, mfanyakazi wa serikali anayeishi 
Plaines Wilhems, katikati mwa Mauritius, anaamka saa tisa usiku 
kusubiri maji ya gari kutoka Mamlaka ya Maji kuweza kupata maji 
ya kupikia na shughuli nyingine za nyumbani. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Kuishi kwa Mlo Mmoja kwa Siku Nchini Swaziland
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4057
</link>
<description>
MBABANE&#044; Aprili 23 &#040;IPS&#041; &#045; Margaret Gamedze anaendesha maisha kwa kupiga pasi 
katika jumuiya yake ya makazi duni ya Msunduza, ambayo 
yanapatikana kilomita moja nje ya mji mkuu wa Swaziland wa 
Mbabane. Tangu mgogoro wa kifedha nchini humo, hawezi tena 
kuingiza fedha ya kuweza kulipia pango katika kijumba chake cha 
tope cha chumba kimoja, ambacho anatumia pamoja na watoto wake 
watano. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Kuokoa Mahindi Nchini Kenya
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4056
</link>
<description>
NAIROBI&#044; Aprili 23 &#040;IPS&#041; &#045; Wakati baadhi ya wakulima wa mahindi katika Jimbo 
la Magharibi nchini Kenya wanaishi kwa kutegemea mavuno ya msimu 
uliopita, Robert Oduor anahesabu hasara yake baada ya magugu 
vamizi yanayojulikana kama Striga au Kayongo kushambulia hekta 
yake moja ya mahindi. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Kudhalilisha Mazungumzo ya Kimataifa ya Biashara
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4055
</link>
<description>
GENEVA&#044; Aprili 19 &#040;IPS&#041; &#045; India, Brazili, na Afrika Kusini, kundi linalokuza 
ushirikiano wa kimataifa miongoni mwa nchi hizo tatu unaojulikana 
kama IBSA, pamoja na China na nchi kadhaa zinazoendelea, 
wamekemea jitihada zinazoendelea za kujaribu kuandaa mikataba ya 
kipekee ya biashara huria ya sekta ya huduma bila kukamilisha 
mazungumzo ya biashara ya kimataifa ya Shirika la Biashara 
Ulimwenguni. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Mto Limpopo Unapogeuka Kuwa Vumbi
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4054
</link>
<description>
BEITBRIDGE, Zimbabwe&#044; Aprili 19 &#040;IPS&#041; &#045; Chapita Ramovha anakumbuka siku ambazo Mto Limpopo 
ulipozingira kijiji chake kusini mwa Zimbabwe. Anasema kuwa hapo 
kabla wakazi wa kijiji cha Makakavhule ilibidi kujenga ukuta 
mrefu kulinda makazi yao kutokana na mafuriko. &quot;Mto Limpopo 
ni kitu cha kushangaa, uzuri wa asili, chanzo cha chakula na 
kipato kwa ajili yetu sisi ambao tunaishi kandokando ya mto 
huo,&quot; anakumbuka mkulima huyo mdogo mdogo. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Bado Wanaume Nchini Ivory Coast Wana Maamuzi Katika Haki za Uzazi
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4053
</link>
<description>
ABIDJAN&#044; Aprili 19 &#040;IPS&#041; &#045; &quot;Ningependa kutumia njia za uzazi wa mpango, 
lakini mume wangu hataki,&quot; anasema Bintou Moussa*. Mama huyo 
mwenye umri wa miaka 32 ndiyo tu anatoka kujifungua mtoto wake wa 
sita katika Hospitali Kuu ya Abobo katika mji maarufu kibiashara 
wa Ivory Coast, Abidjan. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Somo la Demokrasia Katika Mawimbi ya Utangazaji Sudan Kusini
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4052
</link>
<description>
JUBA&#044; Aprili 19 &#040;IPS&#041; &#045; Ni muda wa alasiri na kundi la wanaume na wanawake 
wanaanza kukusanyika chini ya kivuli cha mwembe mkubwa katika mji 
wa Yambio, mji mkuu wa jimbo la maghari mwa Ikweta. Kikundi hiki 
hakipo hapa kwa ajili ya mkutano wa kikabila, kisiasa wala 
masuala ya kidini. Wapo hapa kusikiliza redio. 
</description>
</item>
</channel>
</rss>

