<?xml version="1.0" ?>
<rss version="2.0">
<channel>
<description> </description>
<link>http://www.ipsinternational.org/africa/sw/</link>
<title>  IPS Swahili  </title>
<managingEditor>mgutierrez@ips.org (Miren Gutierrez)</managingEditor>
<webMaster> newsletters@ipsnews.net (Walter Garcia)</webMaster>
<language>SW-sw</language>
<image>
<title>  IPS Swahili  </title>
<url>http://www.ipsinternational.org/africa/sw/../../logo_ips.gif</url>
<link>http://www.ipsinternational.org/africa/sw/</link>
<width>100</width>
<height>42</height>
</image>
<item>
<title>
TANZANIA: Klabu za Vijana, Ufumbuzi wa Changamoto za Watu, Afya na Mazingira
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4263
</link>
<description>
PANGANI&#044; May 6 &#040;IPS&#041; &#045; Sensa ya Idadi ya Watu na Makazi ya mwaka 2002 
ilionyesha kwamba idadi 
ya watu Tanzania iliongezeka kutoka 
milioni 23.1 mnamo 1988 hadi milioni 
34.4 mnamo 2002, ikiwa ni 
wastani wa kiwango cha ukuaji cha asilimia 2.9 
kwa mwaka. Sehemu 
ya watu wenye umri chini ya miaka 15 ilikuwa karibu 
asilimia 44, 
kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Idadi ya Watu 2006. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Timbuktu Yarejesha Hazina Zake
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4262
</link>
<description>
PARIS,&#044; May 2 &#040;IPS&#041; &#045; Pamoja na hali tata na vita vinavyoendelea, Mali 
itafanya kazi ya kujenga na kulinda urithi wake wa kitamaduni, 
anasema waziri wa utamaduni wa taifa hilo la Afrika Magharibi 
Bruno Ma&#239;ga. Ma&#239;ga alikuwa mjini Paris akihudhuria &quot;siku ya 
mshikamano na Mali&quot; iliyoandaliwa na Shirika la Umoja wa 
Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) katika makao yake 
makuu hapa. Tukio hilo lilikusanya pamoja wataalam wa masuala ya 
utamaduni, wakuu wa serikali, wanasanaa na wasomi kutathmini 
uharibifu uliofanyika katika maeneo ya urithi wa kitamaduni ya 
Mali na maandiko ya kizamani, na kuandaa mpango wa kuchukua 
hatua. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Maswali na Majibu: Redio yawapatia Sauti Vijana wa Adeika Kusini - Gives a Voices to South African Youth
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4261
</link>
<description>
UMOJA WA MATAIFA&#044; May 2, &#040;IPS&#041; &#045; Lesedi Mogoatlhe amejitolea maisha yake katika 
kuwawezesha vijana wa Afrika kwa kuwafanya sauti zao zisikike 
kupitia uandishi wa habari wa redio.Katika wakati wa changamoto 
za kiuchumi, kisiada na kitamaduni, vijana wa Afrika Kusini 
wanakabiliwa na masuala magumu mno. Wakiwa vijana wadogo 
wanahofia juu ya mustakabali wa marafiki zao, familia, elimu na 
maisha ya jamii, lakini wakiwa kama Waafrika Kusini pia 
wanakabiliwa na ukweli wa umaskini mkubwa, magonjwa na ghasia. 

</description>
</item>
<item>
<title>
Uwazi Unaweza Kuimarisha Sera za Kukabiliana na Ukame
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4260
</link>
<description>
GENEVA&#044; Machi 15 &#040;IPS&#041; &#045; Wanasayansi waliokusanyika mjini Geneva kwa ajili 
ya Mkutano wa Kwanza wa Watu Maarufu kuhusu Sera za Ukame (HMNDP) 
katika kipindi cha miaka zaidi ya 30 iliyopita walibainisha 
ukusanyaji wa takwimu na usambazaji wa taarifa kama moja ya 
changamoto kubwa za kuzuia ukame kikamilifu. Pia walisema kuwa na 
malengo sahihi na dhamira ya kisiasa yenye nguvu itakuwa muhimu 
katika kujenga sera katika ngazi ya kitaifa. Waliyasema haya 
katika mkutano ambao uliandaliwa kwa pamoja na Taasisi ya Umoja 
wa Mataifa ya Kuzuia Kuenea kwa Jangwa (UNCC), Shirika la Chakula 
Duniani (FAO) na Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO), kati ya 
Machi 11-15 kujaribu kuanzisha mjadala wa kimataifa juu ya sera 
za kitaifa. 
</description>
</item>
<item>
<title>
ANGOLA: Paneli za Jua Zabadili Maji Machafu Kuwa Masafi
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4259
</link>
<description>
LUANDA&#044; Machi 8 2012  &#040;IPS&#041; &#045; Kontena lililopigwa rangi nzuri huku likiwa na 
paneli za jua katika paa lake na vifaa vya kuchujia maji 
linaonekana katika kijiji hiki cha vumbi cha Bom Jesus, kama 
kilomita 50 mashariki mwa mji mkuu wa Angola, Luanda. 
</description>
</item>
<item>
<title>
TANZANIA: Mabadiliko ya Tabia Nchi Yanahitaji Kubadili Mazao ya Kilimo
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4258
</link>
<description>
PANGANI&#044; Machi 7 &#040;IPS&#041; &#045; Kuendelea kwa ukame unaotokana na mabadiliko ya 
tabia nchi katika vijiji vya Mwembeni na Sange wilayani Pangani 
mkoani Tanga kumesababisha kuzidi kupungua kwa upatikanaji wa 
chakula na hivyo kutishia maisha ya wakazi wa vijiji hivyo. 
Lakini mradi wa Pwani unaofadhiliwa na shirika la USAID umeamua 
kuingilia kati kusaidia kunusuru maisha ya wakazi hao na vipato 
vyao. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Mafanikio ya Afrika Kwenye Usalama wa Chakula
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4257
</link>
<description>
NAIROBI&#044; Jan 20 2012 &#040;IPS&#041; &#045; Idadi kubwa ya nchi za Afrika zinapata mafanikio 
makubwa katika kutokomeza njaa na umaskini. Ghana, Liberia, 
Malawi, Rwanda, Sierra Leone na Afrika Kusini ni miongoni mwa 
nchi ambazo zimepata mafanikio makubwa katika kufikia malengo 
haya. 
</description>
</item>
<item>
<title>
TANZANIA - Watoaji Huduma za Uzazi wa Mpango wa Kujitolea Wawafikia Wananchi wa Vijijini
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4256
</link>
<description>
PANGANI&#044; FEB 4 &#040;IPS&#041; &#045; Hashim Ali Said ni mtoaji wa huduma za uzazi wa 
mpango katika jamii (CBD) ambaye ana dhamira ya kweli ya kusaidia 
jamii yake katika kijiji cha Mkalamo na vijiji vingine vya 
jirani. &quot;Kuna wakati wanajamii wanakuja kunigongea mlango 
hata saa sita za usiku kutaka niwapatie kondomu kwa ajili ya 
kupanga uzazi na kujilinda na magonjwa ya kujamiiana,&quot; 
anasema Said mwenye umri wa mika 42.
</description>
</item>
<item>
<title>
Wakazi wa Makazi Duni Wasema &quot;Hapana &quot; kwa Fedha za Damu - Slum Dwellers Say &quot;No&quot; to Blood Money
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4254
</link>
<description>
NAIROBI&#044; Jan 10 &#040;IPS&#041; &#045; Huku ikiwa imebakia miezi miwili kabla Wakenya 
hawajapiga kura kwa kile kinachoonekana kama uchaguzi wenye 
ushindani mkubwa na uliogawanyika sana katika historia ya nchi, 
wengi wanahofia kuwa taifa hili la Afrika Mashariki lenye wakazi 
wanaozidi milioni 40 hawajaona kumalizika kwa ghasia za uchaguzi. 
Hii inajitokeza pamoja na kwamba wanasiasa wawili maarufu - Uhuru 
Kenyatta na William Ruto - bado wanasubiri hatma yao katika 
Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita (ICC) wakikabiliwa na 
uhalifu dhidi ya ubinadamu wakati wa ghasia za baada ya uchaguzi 
mwaka 2007-2008.
</description>
</item>
<item>
<title>
Dawa ya Morphine Inaondoa Maumivu Lakini Bei Inaua Wagonjwa
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4231
</link>
<description>
BULAWAYO&#044; Januari 23, 2013 &#040;IPS&#041; &#045; Iliwachukua mabinti wa Gily Ncube wiki mbili kuuza 
kuku wa kutosha kupata dola 18 zinazohitajika kununulia vidonge 
vya dawa aina ya morphine ambavyo mama yao anakunywa kila baada 
ya masaa manne. Katika nchi ambapo ukosefu wa ajira unakadiriwa 
kuwa asilimia 70, dola 18 kwa kichupa cha vidonge 60 vya uzito wa 
miligramu 10 kila kimoja ni bei kubwa sana kulipia, ikiwa sawa na 
bei ya mikate 18. 

</description>
</item>
<item>
<title>
Maswali na Majibu: Zana Nyingine ya Kupambana na Tohara Duniani
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4230
</link>
<description>
UMOJA WA MATAIFA&#044; Januari 23, 2013 &#040;IPS&#041; &#045; Kwa wastani wa watoto wa kike na wanawake milioni 
140 wanaoishi wakiwa wamefanyiwa tohara (FGM), inaonekana ni 
kuchelewa kuchukua hatua. Lakini tangu dunia ipige marufuku FGM 
mwishoni mwa mwaka jana, wanaharakati wana matumaini kuwa wengi 
wa watoto wa kike na wanawake wataepukana na kitendo hiki cha 
kinyama. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Kesi ya Kukomesha Hukumu ya Kifo Nchini Gambia Yaangukia katika Mahakama Isiyokuwa na Meno
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4228
</link>
<description>
BANJUL&#044; Januari 4 &#040;IPS&#041; &#045; Mahakama ya jumuiya ya kiuchumi katika Afrika 
magharibi inatarajiwa kusikiliza kesi ya kiraia inayotaka 
kukomeshwa kwa hukumu ya kifo nchini Gambia mwezi huu wa Desemba, 
miezi minne baada ya kunyongwa kwa wafungwa tisa na hivyo 
kuushtua ulimwengu.Umoja wa Vyama vya Kiraia Gambia (CSAG), ambao 
unahusisha vikundi kadhaa vya vugugu ya demokrasia, ulipeleka 
kesi hiyo kwa Mahakama ya Jumuiya ya Kiuchumi ya Afrika Magharibi 
(ECOWAS), ambayo ina mamlaka ya kutoa maamuzi juu ya ukiukwaji wa 
haki za binadamu. Mahakama hiyo iko wazi kwa watu wote kutoka 
jumuiya ya ECOWAS, ambayo Gambia ni mwanachama. 
</description>
</item>
<item>
<title>
Mwaswali na Majibu: Kutegemea Demokrasia Kuleta Maendeleo Endelevu
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4227
</link>
<description>
BULAWAYO&#044; Januari 4 &#040;IPS&#041; &#045; &quot;Kukuza shinikizo la kimazingira na kuongezeka 
kukosekana usawa kiuchumi kunazidisha mabadiliko makubwa ya 
kijamii duniani, na hivyo kuifanya demokrasia iliyopo kuingia 
katika majaribu,&quot; Halina Ward, mkurugenzi wa shirika lenye 
makao yake mjini London la &quot;Foundation for Democracy and 
Sustainable Development&quot;, anaiambia IPS. 

</description>
</item>
<item>
<title>
Maswali na Majibu: : &quot;Ni Wakati wa Kupigana Vita ya Ubaguzi wa Ushoga&quot;
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4226
</link>
<description>
UMOJA WA MATAIFA&#044; Januari 4 &#040;IPS&#041; &#045; Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, mwimbaji wa 
kimataifa na mwanaharakati wa haki za binadamu Yvonne Chaka Chaka 
amekuwa mstari wa mbele katika muziki wa pop nchini Afrika 
Kusini. 

</description>
</item>
<item>
<title>
Ndoto za &#8216;Mpango wa Kijani&#8217; Zafifia Katika Maghreb
</title>
<link>
http://www.ipsinternational.org/africa/sw/nota.asp?idnews=4224
</link>
<description>
BERLIN&#044; Januari 3 &#040;IPS&#041; &#045; Mpango wa Viwanda wa Desertec (DII), umoja wa 
makampuni makubwa 21 ya Ulaya, mpango wa kwanza kufunga mtandao 
wa mitambo ya kuzalisha umeme wa mvuke, umeme wa jua, na umeme wa 
upepo katika ukanda mzima wa Maghreb katika Afrika ya Kaskazini, 
ulipokelewa kama &#8216;mpango wa kijani&#8217;. Ukitarajiwa kuzalisha 
gigawati za umeme 100 ifikapo mwaka 2050, mradi ulihitaji 
uwekezaji wa euro bilioni 400. 

</description>
</item>
</channel>
</rss>
