Inter Press Service News Agency
Friday, September 03, 2010   11:04 GMT    
   Homepage
   World Service
   East Africa
   Southern Africa
   West Africa
   Central Africa
 
   Environment
   Health-HIV/AIDS
   Education
   Rights
   Politics
   Economics
   and Finance
   Development
   Energy
   Population
   Culture
 
   Radio Service
 
   Français
 
   About IPS
 
   ENGLISH
   ESPAÑOL
   FRANÇAIS
   ARABIC
   ČESKY
   DEUTSCH
   ITALIANO
   JAPANESE
   MAGYAR
   NEDERLANDS
   POLSKI
   PORTUGUÊS
   SUOMI
   SVENSKA
   SWAHILI
PrintSend to a friend
Readers Opinions

AFRIKA
Kuongezeka kwa Matumizi ya Simu za Mkononi katika Kupanga Uzazi
Susan Anyangu

KAMPALA, Nov 19 (IPS) - Kuongezeka kwa matumizi ya simu za mkononi, hasa katika nchi zinazoendelea, kunawapatia wataalam wa afya aina mpya ya mawasiliano kutoa taarifa za uzazi wa mpango.

"Idadi ya watumiaji wa simu za mkononi inazidi kuongezeka kwa kasi huku idadi ya watumiaji wa simu hizo duniani ikikadiriwa kufikia bilioni 2.6 mwaka 2006 kati ya wakazi bilioni 6.6," anasema David Cantor, meneja ufundi mkuu katika kampuni ya ICF Macro nchini Marekani.

"Takwimu hizi zinatarajiwa kuongezeka hadi bilioni 3.3 au wastani wa nusu ya idadi ya watu wote duniani ifikapo mwaka 2010, huku ongezeko kubwa likiwa barani Asia, Mashariki ya Kati na Afrika."

Cantor, ambaye alikuwa akihudhuria Mkutano wa Kimataifa wa Uzazi wa Mpango mjini Kampala, Uganda Nov. 15-18, anasema kuna ongezeko la nia ya sekta ya afya katika kuwekeza kwenye mawasiliano haya yanayokua kwa kasi.

Kampuni ya One World's Mobile4Good nchini Kenya inatumia teknolojia ya simu za mkononi kuwapa taarifa watumiaji kuhusu fursa za kupima au kupata tiba bure, na pia kutoa huduma ya maswali na majibu ambayo yanaruhusu watu mmoja mmoja kuuliza maswali nyeti ya kiafya.

Nchini Afrika Kusini na Botswana, teknolojia ya simu za mkononi inatumika kukumbusha watu wanaohitaji kupata dawa mara kwa mara.

Jamaica Corker wa shirika la Population Services International (PSI) – programu ya afya ya kimataifa inayolenga katika kupambana na malaria, maisha ya watoto, VVU/UKIMWI na afya ya uzazi – anasema mradi katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo ambako watumiaji wa simu za mkononi wanatumia laini ya bure kupata taarifa zinazohusiana na uzazi wa mpango kumeonyesha nguvu ya teknolojia ya simu za mkononi.

Tangu mwaka 2005, PSI imekuwa ikiendesha laini ya simu za bure ambapo wapigaji wanaweza kuzungumza na waelimishaji na kupata taarifa sahihi kuhusu uzazi wa mpango, au kupelekwa kwenye kliniki au famasi ya karibu, katika eneo ambalo mpiga simu anapatikana.

"Wakati ndiyo inaanza tu, mradi una lengo la kufikia wanawake zaidi, tumeshajifunza kuwa teknolojia ni njia inayofaa kufikia watu kwa ujumbe wa uzazi wa mpango," Corker anasema.

"Kutokana na kwamba wanaume ni idadi kubwa ya watumiaji wa simu za mikononi, wengi wanapiga kwa niaba ya wake zao au marafiki zao wa kike na tunafikisha ujumbe kwao pia."

Matumizi ya laini ya simu za bure ya PSI kwa wanaume wanaotaka taarifa za uzazi wa mpango kunaweza kuonyesha kuongezeka kwa nia ya uzazi wa mpangp miongoni mwa wanaume, pengine kutokana na usiri wa mawasiliano kwa kutumia simu za mkononi.

Kutokana na teknolojia ya simu za mkononi kushuka kwa kasi, Cantor anasema jukwaa limewekwa kwa ajili ya maendeleo ya kasi katika sekta.

Mbali ya kutoa taarifa za uzazi wa mpango, simu za mkononi zinatumiwa kama vyombo vya kufuatilia wagonjwa. Simu za mkononi pia zinatumika kukusanya takwimu za jamii na kliniki, kwa ajili ya kupeleka taarifa kwa wafanyakazi wa afya, watafiti na wagonjwa, na kufuatilia dalili muhimu za mgonjwa. (END/2009)

 

 








 Latest News from Africa
News in RSS
Revolution in African Agriculture Gathering Momentum
Uganda Could Become Regional Rice Exporter say Researchers
Further Victims Identified in DRC Mass Rapes Case
Funding Begins Flowing for African Agriculture
BOTSWANA: HIV-positive Mothers Not Convinced to Exclusively Breastfeed
SOUTH AFRICA: "Xenophobia Simmering Just Below Boiling Point"
Fisheries Can Play Key Role in Africa
SOUTHERN AFRICA: Growing Seed Security
RWANDA: Genocide Ideology and Sectarianism Laws Silencing Critics?
AFRICA: ‘Welcome to My Taxi – Let's Do Business with My Cell Phone'
More >>
  Dernières Nouvelles
News in RSS
Revolution in African Agriculture Gathering Momentum
Uganda Could Become Regional Rice Exporter say Researchers
Further Victims Identified in DRC Mass Rapes Case
Funding Begins Flowing for African Agriculture
BOTSWANA: HIV-positive Mothers Not Convinced to Exclusively Breastfeed
A lire également>>