Inter Press Service News Agency
Saturday, July 31, 2010   23:09 GMT    
   Homepage
   World Service
   East Africa
   Southern Africa
   West Africa
   Central Africa
 
   Environment
   Health-HIV/AIDS
   Education
   Rights
   Politics
   Economics
   and Finance
   Development
   Energy
   Population
   Culture
 
   Radio Service
 
   Français
 
   About IPS
 
   ENGLISH
   ESPAÑOL
   FRANÇAIS
   ARABIC
   ČESKY
   DEUTSCH
   ITALIANO
   JAPANESE
   NEDERLANDS
   POLSKI
   PORTUGUÊS
   SUOMI
   SVENSKA
   SWAHILI
PrintSend to a friend
Readers Opinions

Usawa
Sauti za wanawake zilikuwa na uzito
Na Zarina Geloo

NAIROBI, Januari 25 (IPS) - Vuguvugu la wanawake lilikuwa na sauti nzito wakati wa mkutano wa 2007 wa Nairobi kuliko ilivyokuwa kwenye kongamano nyingine ambazo zimekuwa zikifanya juhudi kuhusisha maswala yake na mambo mengine. Amesema jana Fatma Aloo ambaye pia ni mwanachama wa kamati ya Kongamano linaloangazia aswala ya kijamii.

Aloo ambaye pia ni Afisa mwanachama wa ngazi ya juu wa FEMNET, aliambia mkutano wa Wanahabari siku ya Jumatano kwamba, sauti za wanawake barani Afrika ilikuwa na uzito mkubwa na wazi wakati wa kongamano hili.

''Tofauti na ilivyokuwa kwenye mikutano mingine ambapo sauti zetu zilidhalilishwa na mivumo ya makundi mengine yenye uzito, hapa Nairobi, tulikuwa na zito mkubwa. Tulikuwa na waakilishi kutoka kila pembe, tuliweza kuhusisha maswala yetu na mambo mengine kama vile ardhi, maji na Afya, na muhimu sana, hatukujadili kuhusu kubadilishwa. Tulishauriana na makundi mengine ambayo hayakuwa na utaratibu wa agenda katika kazi zake.''

Aloo, kutoka taifa la Tanzania alisema kumekuwa na mazungumzo mengi na wakati umefika kuonyeshwa kwa vitendo ''Ni lazima tujiondoe kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali na kuwa watendaji.

Kwa sasa, tumefahamu tunachofaa kutenda na jinsi ya kukitenda. Sasa, ni lazima tuchukue hatua za kutenda kisha turudi nyuma na kuripoti maendeleo tuliyopata'' Alisema vuguvugu na makundi yote yataondoka jijini Nairobi yakiwa na mpango wa utekelezaji ambao utatekelezwa kitaifa na kimaeneo.

Wahu Kaara kutoka kitengo kinachohamasisha jamii cha WSF 2007 alisema mashirika yanayohudu nyanjani nchini Kenya yalikuwa yameimarishwa.

''Labda hili ni kongamano la kipekee watakalohudhuria kwani liko katika eneo lao na wametumia nafasi yote ipasavyo.

Walifafanua vyema visa vyao, wakatangamana na makundi mengine na kubuni mtandao thabiti ambao utawapeleka mbali hata baada ya mkutano,'' akasema Kaara.

Alisema mazungumzo kuhusu wanawake katika maeneo yanayokabiliwa na vita hasa Somalia na Darfur yalikuwa ya kuvunja moyo kwani akina mama wengi aliaothiriwa na mapigano hawakuweza kuhudhuria na kusimulia visa vyao. Hata hivyo, maswala yao yalijadiliwa na makundi yenye mshikamano yaliyokuwa yakifanya kazi maeneo hayo. (END/2007)

 

 








 Latest News from Africa
News in RSS
BURKINA FASO: Race to Achieve Goals on Sanitation
MALAWI: Innovative Campaigning by Women Candidates
SOUTHERN AFRICA: Realising Trade in Virtual Water
KENYA: Claim Disputed that Trade Measures "Aid" Counterfeiters
POLITICS-GUINEA: Women Amongst Also-Rans in Presidential Elections
ZIMBABWE: Badly Needed Work Begins on Bulawayo Water System
MADAGASCAR: Women Form Own Political Parties for Fair Representation
HEALTH: Uganda Authority Finding Less Counterfeit Drugs
TRADE-NAMIBIA: EU Backs Off on EPA
TRADE: Malawi Stands Firm on Conditions for Signing EPA
More >>
  Dernières Nouvelles
News in RSS
BURKINA FASO: Race to Achieve Goals on Sanitation
MALAWI: Innovative Campaigning by Women Candidates
SOUTHERN AFRICA: Realising Trade in Virtual Water
KENYA: Claim Disputed that Trade Measures "Aid" Counterfeiters
POLITICS-GUINEA: Women Amongst Also-Rans in Presidential Elections
A lire également>>