Usawa Sauti za wanawake zilikuwa na uzito Na Zarina Geloo
NAIROBI, Januari 25 (IPS) - Vuguvugu la wanawake lilikuwa na sauti nzito wakati wa
mkutano wa 2007 wa Nairobi kuliko ilivyokuwa kwenye kongamano nyingine
ambazo
zimekuwa zikifanya juhudi kuhusisha maswala yake na mambo mengine. Amesema
jana Fatma Aloo ambaye pia ni mwanachama wa kamati ya Kongamano
linaloangazia aswala ya kijamii.
Aloo ambaye pia ni Afisa mwanachama wa ngazi ya juu wa FEMNET, aliambia
mkutano wa Wanahabari siku ya Jumatano kwamba, sauti za wanawake barani
Afrika ilikuwa na uzito mkubwa na wazi wakati wa kongamano hili.
''Tofauti na ilivyokuwa kwenye mikutano mingine ambapo sauti zetu
zilidhalilishwa na mivumo ya makundi mengine yenye uzito, hapa Nairobi,
tulikuwa na zito mkubwa. Tulikuwa na waakilishi kutoka kila pembe, tuliweza
kuhusisha maswala yetu na mambo mengine kama vile ardhi, maji na Afya, na
muhimu sana, hatukujadili kuhusu kubadilishwa. Tulishauriana na makundi
mengine ambayo hayakuwa na utaratibu wa agenda katika kazi zake.''
Aloo, kutoka taifa la Tanzania alisema kumekuwa na mazungumzo mengi na
wakati umefika kuonyeshwa kwa vitendo ''Ni lazima tujiondoe kutoka mashirika
yasiyo ya kiserikali na kuwa watendaji.
Kwa sasa, tumefahamu tunachofaa kutenda na jinsi ya kukitenda. Sasa, ni
lazima tuchukue hatua za kutenda kisha turudi nyuma na kuripoti maendeleo
tuliyopata'' Alisema vuguvugu na makundi yote yataondoka jijini Nairobi
yakiwa na mpango wa utekelezaji ambao utatekelezwa kitaifa na kimaeneo.
Wahu Kaara kutoka kitengo kinachohamasisha jamii cha WSF 2007 alisema
mashirika yanayohudu nyanjani nchini Kenya yalikuwa yameimarishwa.
''Labda hili ni kongamano la kipekee watakalohudhuria kwani liko katika eneo
lao na wametumia nafasi yote ipasavyo.
Walifafanua vyema visa vyao, wakatangamana na makundi mengine na kubuni
mtandao thabiti ambao utawapeleka mbali hata baada ya mkutano,'' akasema
Kaara.
Alisema mazungumzo kuhusu wanawake katika maeneo yanayokabiliwa na vita hasa
Somalia na Darfur yalikuwa ya kuvunja moyo kwani akina mama wengi
aliaothiriwa na mapigano hawakuweza kuhudhuria na kusimulia visa vyao. Hata
hivyo, maswala yao yalijadiliwa na makundi yenye mshikamano yaliyokuwa
yakifanya kazi maeneo hayo. (END/2007)
|
|
|