Tahariri - Mario Lubetkin Changamoto za mkutano wa Nairobi
NAIROBI, Januari 23 (IPS) - Tumewasili katika mkutano wa saba wa maswala ya
kijamii, kongamano la kwanza kabisa kuandaliwa Barani Afrika. Tumeshuhudia
ufanisi wa mikutano mingine minne iliyoandaliwa Porto Alegre, Brazil na huko
Mumbai India. Mnamo mwaka wa 2006, tulishiriki katika mkutano wa kwanza
ulioandaliwa Bamako, Caracas na Karachi.
WSF imedhihirisha uwezo na nguvu zake miaka iliyopita kwa kuhamasisha
mikutano ya maelfu ya watu kimaeneo, kimataifa na kutoka pembe mbali mbali
za dunia na kupelekea kuwepo kwa matarajio na matumaini miongoni mwa
mamilioni ya watu kote ulimwenguni, kwamba 'ulimwengu mwingine
unawezekana''. Mikakati muhimu imeibuka kutoka WSF kama vile kuandaa juhudi
za pamoja mwaka wa 2003 kuhusiana na amani, kupinga vita na kampeini
iliyofana sana iliyozinduliwa mwaka wa 2005 kupambana na umaskini.(GCAP).
Baada ya miaka 7, maswali mapya yameibuka kuhusiana na hali ya baadaye ya
WSF. Je, vuguvugu hili linaelekea wapi?Je, malengo yake ya baadaye ni yapi?
Je, vuguvugu hili litakabiliana vipi na mabadiliko makubwa na kuwa na
matumaini? Kila mmoja wetu anaweza kuwa na maswali mapya lakini ni muhimu
kuangazia matumaini ya baadaye ya WSF.
Ni kwa sababu hiyo ambapo mashirika mengi mojawapo likiwa IPS linalokuletea
TerraViva limekubali kujihusisha na shughuli mbali mbali zinazoangazia siku
za
awali za WSF, Nairobi. Madhumuni yake ni kufahamu yaliyotendeka miaka
iliyopita kuhusiana na WSF, wajibu wa wanaharakati wa kijamii na kwa mujibu
huu
wajibu wa mikutano na pia uhusiano wake na mifumo ya kisiasa kwa kuzingatia
serikali nyingi zilizoibuka tangu mwaka wa 2001 chini ya wafuasi wa WSF.
Sio tu kwa kupata majibu mahsusi lakini kwa kubuni taratibu za kujadiliwa
baada ya mkutano wa Nairobi. Mawasiliano lazima yachukue nafasi muhimu
katika mjadala huu ulio wazi na wa haki. Ni kwa sababu hiyo ndipo tumefanya
kazi na mashirika rafiki kuandaa mkutano wa tatu wa kimataifa kuhusu habari
na mawasiliano chini ya muktadha wa WSF, kuzidi kuimarisha ufahamu kuhusu
mawasiliano na kwa jumla jamii nzima.
Lakini , kwa wakati huo, lazima tuwe na vyombo vya mawasiliano
vitakavyotuwezesha kuangazia hatua za kuanzia mjini Nairobi. Kama
ilivyokawaida, IPS, itatekeleza wajibu wake. Kwa washiriki wote wa kongamano
la IPS mjini Nairobi , endeleeni kusoma jarida la TerraViva! (END/2007)
|
|
|