NGUZU ZA WATU Kutumia Michoro Na Martin Adhola
NAIROBI, Januari 23 (IPS) - Mbinu za hapo awali za kutumia michoro kuwasiliana na
kutoa hisia zimefufuliwa tena. Vijana kutoka mataifa sita ambayo ni Kenya,
frika Kusini, Colombia, Switzerland, Tanzania na Mozambique walitumia mbinu
za hapo kale kuwasiliana kuhusu hisia zao za ndani, kupasha ujumbe kuhusu
Ukimwi, amani, kuwezesha na maendeleo.
Huku wakiandaa onyesho lao la kwanza wakati wa mkutano unaongazia maswala ya
kijamii, vijana hao wanaohudumu chini ya aegis of The Terres des Homes
hweiz,
ambalo ni shirika la maendeleo la Uswizi walisema waliamua kutumia mbinu za
jadi za mawasiliano ili kupitisha ujumbe wao.
Raisa Bonjour kutoka Uswizi alisema hii ilikuwa mbinu ya kipekee ya
kuwasiliana kuonyesha hisia za ndani: ''Ni chombo muhimu kwa vijana
kuwasiliana baina ao ili kuelezea hali mbali mbali wanazopitia kila siku''.
Ikiwa imetumika kutoka michoro ya mawe ya zamani Barani Afrika, michoro hii
imechapwa urembo kwa
kutumia rangi na nta (batiki) hali ambayo bali na kudhihirisha teknolojia
inadumisha njia za mawasiliano.
Irene Bush ambaye ni Mkurugenzi alisema mradi ulifaulu kuwashirikisha
vijana: ''Michoro tunayoiona siku hizi ni taarifa muhimu kuhusu maisha ya
vijana''.
Vijana hao 12 walitoa taswira kuhusu yaliyopita, yaliyomo na yanayotarajiwa
kuhusiana na sanaa ya uchoraji. Bw. Robert Ngatia kutoka mradi wa pamoja wa
Kasarani (Kasarani Intergrated Programme) alisema ''hiki ni chombo rahisi na
muhimu cha kuwasiliana ambacho kinaweza kuimarishwa na vijana ili
kuwasilisha
ujumbe kuhusu wanavyojihisi na wakati huo kutoa hisia zao za ndani''. (END/2007)
|
|
|