NGUZU ZA WATU Kutoka majengo ya mabanda hadi ulimwengu mwingine Na Joyce Mulama
NAIROBI, Januari 25 (IPS) - Waliandamana kutoka makao ya mabanda yaliyo makubwa
zaidi kanda hii hadi Bustani ya Uhuru kutangaza kwamba ''Ulimwengu mwingine
unawezekana'' na wakati huo kuzindua mkutano wa saba kuhusu maswala ya
kijamii (WSF) siku ya Jumamosi.
Kongamano hili lililoanza Januari 20 hadi 25 limejumuisha pamoja maelfu ya
wajumbe kutoka pembe zote za dunia ili kuweka pamoja ''haki za kijamii,
umoja wa kimataifa, usawa wa kijnsia, amani na kuzuia uharibifu wa
mazingira'' katika agenda za kimataifa.
Mkutano kuhusu maswala ya kijamii umewadiwa huku wanaharakati wa kijamii
wakikabiliana na changamoto zinazoibuka kutokana na ''vita dhidi ya
ugaidi'', ukosefu wa usawa kiuchumi unaosababishwa na utandawazi huku
wanaharakati hao wakiombwa kudhihirisha uhalalishaji, uwazi na uwajibikaji.
Washiriki wengi walifurika katika Bustani ya Uhuru huku wakiwa wamevalia
fulana zilizokuwa na maandishi na kupeperusha bendera na mabango baada ya
kufanya maandamano dhidi ya umaskini yaliyoanzia mtaa wa Kibera ulioko
karibu kilomita saba Kusini Magharibi mwa Jiji la Nairobi.
Huku ukiwa na idadi ya watu wapatao elfu 700,000, mtaa huu ndio mkubwa zaidi
katika eneo la Afrika Mashariki. Katika mtaa huu, wajumbe walikumbana ana
kwa a na hali ya kusikitisha ya umaskini, nyumba za matope,harufu mbaya
iliyotokana na maji taka, ukosefu wa maji, barabara au huduma zozote. Katika
Bustani, kila aliyezungumza alishutumu mataifa tajiri kwa kubuni sera
zilizopelekea kuongezeka kwa hali ya umaskini katika mataifa yanayokua.
''Tunafahamu dunia tunayotaka. Dunia isiyotawaliwa na mataifa kutoka
magharibi. Dunia yenye heshima na isiyo na madeni yaliyotokana na utawala
huu.'' Chico Whitaker ambaye ni mwanachama wa Baraza la WSF akasema.
Swala kuhusu ugonjwa hatari wa HIV/AIDS lilichukua nafasi kubwa huku
waliotoa hotuba wakisema janga hili limekuwa changamoto kwa mataifa
yanayoendelea. ''Kuzuia ni bora kuliko kutibu.'' Akasema Rais Mstaafu wa
Zambia Bw. Kenneth Kaunda. ''Ni lazima tukumbuke vituo vya kupimwa kwa hiari
(VCT).
''Kujua hali yako ya afya na kujadili wazi kuhusu swala hili kutapunguza
unyanyapaa. Siwambii jambo ambalo sijalifanya.'' Akasema Rais Kaunda ambaye
alipimwa kwa hiari baada ya mwanawe wa kiume kuaga dunia kutokana na maradhi
ya Ukimwi.
Mkutano wa WSF unaandaliwa chini ya mwito wake ''watu wanajitahidi, njia
badala za watu''. Bw. Oduor Ong'wen ambaye ni mwanachama wa kamati andalizi
ya
mkutano alizungumuza kwa ufupi kuhusu matarajio ya mkutano kwa niaba ya
TerraViva.
''Tunatarajia kwamba watu watajadiliana kuhusu dnuia ya sasa, jinsi ilivyo
na kutafuta njia badala za kuwa na ulimwengu bora''. (END/2007)
|
|
|