Inter Press Service News Agency
Saturday, July 31, 2010   23:13 GMT    
   Homepage
   World Service
   East Africa
   Southern Africa
   West Africa
   Central Africa
 
   Environment
   Health-HIV/AIDS
   Education
   Rights
   Politics
   Economics
   and Finance
   Development
   Energy
   Population
   Culture
 
   Radio Service
 
   Français
 
   About IPS
 
   ENGLISH
   ESPAÑOL
   FRANÇAIS
   ARABIC
   ČESKY
   DEUTSCH
   ITALIANO
   JAPANESE
   NEDERLANDS
   POLSKI
   PORTUGUÊS
   SUOMI
   SVENSKA
   SWAHILI
PrintSend to a friend
Readers Opinions

NGUZU ZA WATU
Kutoka majengo ya mabanda hadi ulimwengu mwingine
Na Joyce Mulama

NAIROBI, Januari 25 (IPS) - Waliandamana kutoka makao ya mabanda yaliyo makubwa zaidi kanda hii hadi Bustani ya Uhuru kutangaza kwamba ''Ulimwengu mwingine unawezekana'' na wakati huo kuzindua mkutano wa saba kuhusu maswala ya kijamii (WSF) siku ya Jumamosi.

Kongamano hili lililoanza Januari 20 hadi 25 limejumuisha pamoja maelfu ya wajumbe kutoka pembe zote za dunia ili kuweka pamoja ''haki za kijamii, umoja wa kimataifa, usawa wa kijnsia, amani na kuzuia uharibifu wa mazingira'' katika agenda za kimataifa.

Mkutano kuhusu maswala ya kijamii umewadiwa huku wanaharakati wa kijamii wakikabiliana na changamoto zinazoibuka kutokana na ''vita dhidi ya ugaidi'', ukosefu wa usawa kiuchumi unaosababishwa na utandawazi huku wanaharakati hao wakiombwa kudhihirisha uhalalishaji, uwazi na uwajibikaji.

Washiriki wengi walifurika katika Bustani ya Uhuru huku wakiwa wamevalia fulana zilizokuwa na maandishi na kupeperusha bendera na mabango baada ya kufanya maandamano dhidi ya umaskini yaliyoanzia mtaa wa Kibera ulioko karibu kilomita saba Kusini Magharibi mwa Jiji la Nairobi.

Huku ukiwa na idadi ya watu wapatao elfu 700,000, mtaa huu ndio mkubwa zaidi katika eneo la Afrika Mashariki. Katika mtaa huu, wajumbe walikumbana ana kwa a na hali ya kusikitisha ya umaskini, nyumba za matope,harufu mbaya iliyotokana na maji taka, ukosefu wa maji, barabara au huduma zozote. Katika Bustani, kila aliyezungumza alishutumu mataifa tajiri kwa kubuni sera zilizopelekea kuongezeka kwa hali ya umaskini katika mataifa yanayokua.

''Tunafahamu dunia tunayotaka. Dunia isiyotawaliwa na mataifa kutoka magharibi. Dunia yenye heshima na isiyo na madeni yaliyotokana na utawala huu.'' Chico Whitaker ambaye ni mwanachama wa Baraza la WSF akasema.

Swala kuhusu ugonjwa hatari wa HIV/AIDS lilichukua nafasi kubwa huku waliotoa hotuba wakisema janga hili limekuwa changamoto kwa mataifa yanayoendelea. ''Kuzuia ni bora kuliko kutibu.'' Akasema Rais Mstaafu wa Zambia Bw. Kenneth Kaunda. ''Ni lazima tukumbuke vituo vya kupimwa kwa hiari (VCT).

''Kujua hali yako ya afya na kujadili wazi kuhusu swala hili kutapunguza unyanyapaa. Siwambii jambo ambalo sijalifanya.'' Akasema Rais Kaunda ambaye alipimwa kwa hiari baada ya mwanawe wa kiume kuaga dunia kutokana na maradhi ya Ukimwi.

Mkutano wa WSF unaandaliwa chini ya mwito wake ''watu wanajitahidi, njia badala za watu''. Bw. Oduor Ong'wen ambaye ni mwanachama wa kamati andalizi ya mkutano alizungumuza kwa ufupi kuhusu matarajio ya mkutano kwa niaba ya TerraViva.

''Tunatarajia kwamba watu watajadiliana kuhusu dnuia ya sasa, jinsi ilivyo na kutafuta njia badala za kuwa na ulimwengu bora''. (END/2007)

 

 








 Latest News from Africa
News in RSS
BURKINA FASO: Race to Achieve Goals on Sanitation
MALAWI: Innovative Campaigning by Women Candidates
SOUTHERN AFRICA: Realising Trade in Virtual Water
KENYA: Claim Disputed that Trade Measures "Aid" Counterfeiters
POLITICS-GUINEA: Women Amongst Also-Rans in Presidential Elections
ZIMBABWE: Badly Needed Work Begins on Bulawayo Water System
MADAGASCAR: Women Form Own Political Parties for Fair Representation
HEALTH: Uganda Authority Finding Less Counterfeit Drugs
TRADE-NAMIBIA: EU Backs Off on EPA
TRADE: Malawi Stands Firm on Conditions for Signing EPA
More >>
  Dernières Nouvelles
News in RSS
BURKINA FASO: Race to Achieve Goals on Sanitation
MALAWI: Innovative Campaigning by Women Candidates
SOUTHERN AFRICA: Realising Trade in Virtual Water
KENYA: Claim Disputed that Trade Measures "Aid" Counterfeiters
POLITICS-GUINEA: Women Amongst Also-Rans in Presidential Elections
A lire également>>